Psalms 3:2-7


2 aWengi wanasema juu yangu,
“Mungu hatamwokoa.”


3 bLakini wewe, Ee Bwana, ni ngao pande zote;
umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.

4 cNinamlilia Bwana kwa sauti kuu,
naye ananijibu kutoka mlima wake mtakatifu.


5 dNinajilaza na kupata usingizi;
naamka tena, kwa maana Bwana hunitegemeza.

6 eSitaogopa makumi elfu ya adui,
wanaojipanga dhidi yangu kila upande.


7 fEe Bwana, amka!
Niokoe, Ee Mungu wangu!
Wapige adui zangu wote kwenye taya,
vunja meno ya waovu.

Copyright information for SwhKC